Thursday 29 May 2014

KARIBUNI TUJIFUNZE JINSI YA KUPIKA NYAMA KWA MTINDO WA KICHINA( BEEF CHINESE STYLE)

       MAHITAJI
-Nyama (beef steak)
-Soy sauce
-Worcester sauce
-Vitunguu(onions)
-Vitunguu swaumu(garlic)
-Tangawizi(ginger)
-Pilipili hoho(green pepper)
-Karoti(carrot)
-Pilipili manga(black pepper)
-Chumvi(salt)
-Mchuzi wa kuku au mchuzi wa nyama au mvinyo mweupe(beef stock, chicken stock or white wine)
-Mafuta ya kula(oil)


      MAANDALIZI YA KUPIKA
-Katakata vitunguu, pilipili hoho na karoti kwa mtindo wa julieni.
-Katakata nyama pia kwa mtindo wa julieni.
-Saga tangawizi pamoja na vitunguu swaumu


      HATUA ZA KUPIKA
-Chemsha nyama
-Baada ya kuiva nyama yako ichuje na ule mchuzi wake weka pembeni
-Weka pan yako jikon na mafuta kidogo na baada ya mafuta kupata moto weka vitunguu maji, vitunguu swaumu, tangawizi na ukaange kwa dakika 3.
-Baada ya hapo weka karoti na pilipili hoho na ukaange kwa dakika 3 na uweke chumvi kidogo.
-Baada ya kuiva hizo mbogamboga weka pembeni pia.
-Baada ya hapo weka pan yako nyingine na uweke mafuta kidogo na uweke vitunguu, vitunguu swaum na tangawizi hivyo vyote weka kwakiasi kidogo.
-Baada ya hapo weka nyama na uikange kidogo na uweke mbogamboga zako, kwakuwa ulishazikaanga hapo awali zinapaswa zisiive san.
-Baada ya hapo weka soy sauce, Worcester sauce na ukologe.
-Baada ya hapo uweka stock yako yaani mchuzi wa kuku au mchuzi wa nyama ya uliohemshia au mvinyo mweupe
-Baada ya weka chumvi pamoja na pilipili manga

ANAGALIA BAADHI YA PICHA
.
























NAWATAKIA CHAKULA CHEMA

AHSANTENI WADAU WANGU

BY IRON CHEF JACKSON


Thursday 22 May 2014

KARIBUNI TUJIFUNZE JINSI YA KUPIKA MCHELE WA BASMAT


        MAHITAJI
 
-Mchele wa basmat(basmat rice)
-Binzari(tumeric)
-Vitunguu(onions)
-Chumvi(salt)
-Maji(water)
-Mafuta ya kura


                 HATUA ZA KUPIKA
-Osha mchele kwa maji mara moja tu
-Weka sufuria pamoja na maji
-Baada ya maji kuchemka weka chumvi pamoja na mchele
-Wakati unauchemsha unatakiwa usiive sana maana utakuwa kama uji(bokoboko)
-Baada ya hapo uchuje mchele na uweke pembeni
-Chukua sufuria yako na uweke mafuta
-Baada ya weka vitunguu vyako ambavyo utakuwa umekata mtindo wa chopchop
-Baada ya vitunguu kuiva weka binzari yako pia na uendelee kukologa ili isishikane
-Baada ya hapo, weka mchele wako ktk sufuri yako yenye vitunguu na binzari
-Baada ya hapo endelea kukologa ili uchanganyikane na viungo
-Baada ya hapo zima jiko na chakula kitakuwa tayari
-Chukua pani yako na uweke mafuta mengi kwa ajili ya kukaanga vitunguu ambavyo utakuwa umekata kwa mtindo wa nusu duara(half ring) na uanze kuvikaanga mpaka upate rangi ya kahawia(brown).
-Baada ya hapo pakuwa wali wako ktk bakuli kubwa na juu yake uweke vitunguu ulivyokaanga
- Hapo chakula tayari kwa kuliwa

NAWATAKIA CHAKULA CHEMA WADAU WANGU

AHSANTEN SANA WADAU WANGU

BY IRON CHEF JACKSON