Thursday 29 May 2014

KARIBUNI TUJIFUNZE JINSI YA KUPIKA NYAMA KWA MTINDO WA KICHINA( BEEF CHINESE STYLE)

       MAHITAJI
-Nyama (beef steak)
-Soy sauce
-Worcester sauce
-Vitunguu(onions)
-Vitunguu swaumu(garlic)
-Tangawizi(ginger)
-Pilipili hoho(green pepper)
-Karoti(carrot)
-Pilipili manga(black pepper)
-Chumvi(salt)
-Mchuzi wa kuku au mchuzi wa nyama au mvinyo mweupe(beef stock, chicken stock or white wine)
-Mafuta ya kula(oil)


      MAANDALIZI YA KUPIKA
-Katakata vitunguu, pilipili hoho na karoti kwa mtindo wa julieni.
-Katakata nyama pia kwa mtindo wa julieni.
-Saga tangawizi pamoja na vitunguu swaumu


      HATUA ZA KUPIKA
-Chemsha nyama
-Baada ya kuiva nyama yako ichuje na ule mchuzi wake weka pembeni
-Weka pan yako jikon na mafuta kidogo na baada ya mafuta kupata moto weka vitunguu maji, vitunguu swaumu, tangawizi na ukaange kwa dakika 3.
-Baada ya hapo weka karoti na pilipili hoho na ukaange kwa dakika 3 na uweke chumvi kidogo.
-Baada ya kuiva hizo mbogamboga weka pembeni pia.
-Baada ya hapo weka pan yako nyingine na uweke mafuta kidogo na uweke vitunguu, vitunguu swaum na tangawizi hivyo vyote weka kwakiasi kidogo.
-Baada ya hapo weka nyama na uikange kidogo na uweke mbogamboga zako, kwakuwa ulishazikaanga hapo awali zinapaswa zisiive san.
-Baada ya hapo weka soy sauce, Worcester sauce na ukologe.
-Baada ya hapo uweka stock yako yaani mchuzi wa kuku au mchuzi wa nyama ya uliohemshia au mvinyo mweupe
-Baada ya weka chumvi pamoja na pilipili manga

ANAGALIA BAADHI YA PICHA
.
























NAWATAKIA CHAKULA CHEMA

AHSANTENI WADAU WANGU

BY IRON CHEF JACKSON


Thursday 22 May 2014

KARIBUNI TUJIFUNZE JINSI YA KUPIKA MCHELE WA BASMAT


        MAHITAJI
 
-Mchele wa basmat(basmat rice)
-Binzari(tumeric)
-Vitunguu(onions)
-Chumvi(salt)
-Maji(water)
-Mafuta ya kura


                 HATUA ZA KUPIKA
-Osha mchele kwa maji mara moja tu
-Weka sufuria pamoja na maji
-Baada ya maji kuchemka weka chumvi pamoja na mchele
-Wakati unauchemsha unatakiwa usiive sana maana utakuwa kama uji(bokoboko)
-Baada ya hapo uchuje mchele na uweke pembeni
-Chukua sufuria yako na uweke mafuta
-Baada ya weka vitunguu vyako ambavyo utakuwa umekata mtindo wa chopchop
-Baada ya vitunguu kuiva weka binzari yako pia na uendelee kukologa ili isishikane
-Baada ya hapo, weka mchele wako ktk sufuri yako yenye vitunguu na binzari
-Baada ya hapo endelea kukologa ili uchanganyikane na viungo
-Baada ya hapo zima jiko na chakula kitakuwa tayari
-Chukua pani yako na uweke mafuta mengi kwa ajili ya kukaanga vitunguu ambavyo utakuwa umekata kwa mtindo wa nusu duara(half ring) na uanze kuvikaanga mpaka upate rangi ya kahawia(brown).
-Baada ya hapo pakuwa wali wako ktk bakuli kubwa na juu yake uweke vitunguu ulivyokaanga
- Hapo chakula tayari kwa kuliwa

NAWATAKIA CHAKULA CHEMA WADAU WANGU

AHSANTEN SANA WADAU WANGU

BY IRON CHEF JACKSON









Monday 17 February 2014

KARIBUNI TUJIFUNZE JINSI YA KUPIKA MCHUZI WA NYAMA AU BEEF STEW

           
                  MAHITAJI
        - Nyama ya ng'ombe (Beef)
        - Soy sauce
        -Vitunguu (onions)
        -Mafuta ya kula( vegetable oil)
        -vitunguu swaumu(garlic)
        - Pilipili hoho(green pepper)
        - Karoti(carrot)
         -Pilipili manga(black powder)
         - mchuzi wa nyama(beef stock or beef broth)
         -Nyanya ya kusaga(Tomato paste)


                   HATUA ZA KUPIKA
          -Katakata nyama kwa mkato wa pembe nne(cubes)
         - Chemsha nyama yako mpaka iive kabisa na vitunguu swaumu
         -Katakata karoti, pilipili hoho, pamoja na vitunguu kwa mkato wa julieni
         -Baada ya nyama yako kuiva weka pembeni na uweke flampeni weka mafuta kiasi kidogo sana
         - Baada ya mafuta kupata moto weka vitungu, pilipili hoho pamoja na karoti na uanze kuangaa(sautee)
         -Wakati naendelea kukaanga weka soy sauce
         -Baaada ya kuiva mbogamboga zako(karoti, vitunguu na pilipili hoho) ipua na uweke pembeni
         -Baada yapo chukua nyama yako ambayo uliichemsha na uichuje na ule mchuzi wako utunze kwaajili              ya baadae.
         -Baada ya hapo chukua nyama flampeni na uweke mafuta kidogo na uikaange
         - Baada ya hapo weka zile mbogamboga zako(karoti, pilipili hoho na vitunguu) yaani uchanganye                     pamoja na nyama yako
         -Baada ya kuchanya mbogamboga zako, weka soy sauce
         -Baada ya hapo weka nyanya yako ya kusaga(tomato paste) na uikologe au kuichanganya pamoja
         - Baada ya weka mchuzi wako uliouchuja kutoka ktk nyama, au mchuzi wa nyama(beef stock or broth
         - Baada ya hapo weka pilipili manga,na chumvi(black pepper and salt)
         -Baada ya hapo punguza moto wako na uiache kwa muda wa dakika 5 tu na uipue
         - Chakula hichi unaweza ukala na wali(rice)
         -Mwishooooooooo

AHSANTEN SANA WADAU WANGU.........!!!!!
 NAWATAKIA CHAKULA CHEMA WAPENDWA............!!!!!!!


ANGALIA HII PICHA...!!!!